Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib
     

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 
ProfileToolsGamesCommunity

NEWS

 
 

Viza ya Tanzania na Afrika Kusini imefutwa

29/10/2010

Imepokewa na Wavuti

Rafiki yangu (Toninho) ananitumia ujumbe jana akiuliza kuhusu kufutwa viza ya Tanzania-Afrika Kusini.

Kwa kuwa sikuwa na majibu kuhusiana na hilo, niliomba msaada wa majibu toka kwa watu kadhaa na mojawapo ni katika ukurasa wangu wa Facebook (marafiki zangu wa hapo watakuwa wameusoma jana).

Ninamshukuru rafiki yangu kaka Ken wa kuthibitisha na kuambatanisha nakala (ninayo) ya barua toka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Investment Center (TIC) akimwandikia Mwenyekiti wa Kamati ya Watanzania Botswana kumfahamisha kuhusu kufutwa kwa viza hiyo.

Sehamu ya barua hiyo inasema,

"Ninayo furaha kuwaletea habari njema kwamba jana tarehe 27 Oktoba 2010, Mhe. Balozi wa Afrika Kusini na Mkuu wa Kitengo cha VISA cha Ubalozi huo wamenijulisha rasmi kwamba kuanzia Novemba Mosi 2010, VISA kati ya Afrika Kusini na Tanzania ZIMEFUTWA.

Hizo ni habari njema za kilio chenu mlichnituma tulipoonana Mjini Gaborone miezi mitatu iliyopita."

 

   
 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
News Archive

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©