Baada ya
siku tano za kusubiri matokeo ya kura
zilizopigwa na wananchi siku ya Jumapili,
Oktoba 31, 2010 ili kumpata mtu
atakayekimiliki kiti cha Urais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
hatimaye matokeo hayo yametolewa na Tume
ya Uchaguzi Tanzania, NEC, katika
viwanja vya Karimjee jijini Dar Es
Salaam. Jakaya Mrisho Kikwete atangazwa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
kwa kuongoza kura asilimia 61.17%.
Habari
na Picha
Mwenyekiti wa Tume ya
Uchaguzi Jaji Lewis Makame alimkabidhi
cheti Mgombea Urais kwa tiketi ya Chama
Cha Mapinduzi Dk. Jakaya Mrisho Kikwete
baada ya kumtangaza kushinda katika mbio
za urais katika uchaguzi wa mwaka 2010.
Hafla hiyo ilifanyika katika viwanja vya
Karimjee jijini Dar es Salaam.
Wagombea
uchaguzi wa Urais 2010

Matokeo kwa mlinganyo wa kura
kwa vyama na wagombezi wake
kuanzia kura zilizo chache mpaka
mshindi wa uchaguzi wa Urais wa
mwaka 2010 ni kama ifuatavyo:
-
Dovutwa Yahmi Nassoro/UPDP
kura 13,176 = 0.15%
-
Mgahywa Muttamwega Bhatt/TLP
kura 17,482 = 0.20%
-
Rungwe Hashim Spunga/NCCR-Mageuzi
kura 26,388 = 0.31%
-
Kuga Peter Mziray/APPT
Maendeleo kura 96,933 =
1.12%
-
Lipumba Ibrahim Haruna/CUF
kura 695,667 = 8.06%
-
Slaa Willibrod Peter/CHADEMA
kura 2,271,941 = 26.34%
-
Kikwete Jakaya Mrisho/CCM
kura 5,276,827= 61.17%