RAMADHAN QURAN CONTEST 2008

Mount Kilimanjaro

Beit El Ajaib

   

 

HomeNewsServicesEventsAbout UsContact Us

 

ProfileToolsGamesCommunity

 

 

Ramadhan Qur'an Contest 2008 - 20/09/2008

 

Mashindano ya pili ya Qur'an (Ramadhan Quran Contest 2008) ambayo yamefanyika tarehe 20/09/2008 yamekuwa ya mafanikio makubwa kama alivyosema Mwenyekiti wa Zenjydar Community Association bwana Saleh Jaber.

Mashindano ya mwaka huu kulinganisha na ya mwaka jana, imeonyesha kuwa na maendeleoa katika mashindano hayo ambayo yameshukuriwa na kamati ya Zenjydar kwa wote waliochangia kufanya mashindano hayo kufanyika. Mwaka huu Zenjydar imealika vyuo vyote kushirikisha watoto wao katika mashindano hayo tangu mwezi wa nne (April 2008) ambayo matokeo yake baadhi ya vyuo vimeshiriki na baadhi ya vyuo vimekutwa na dharura ya kutokushiriki. Vilevile mwaka huu, Zenjydar imetanua mualiko wake wa watoto kushiriki katika mashindano hayo kwa kuwakaribisha wazazi na familia mbalimbali kujisajili na kushiriki katika mashindano hayo na Zenjydar inashukuru jitihada za Waalimu na Wazazi wote ambao wameshiriki na kuwabiidisha watoto wao kushiriki katika mashindano hayo katika mwezi mtukufu wa Ramadhan. Vilevile, shukran kwa wote waliorudisha fomu za mawazo ambazo zilitolewa na Zenjydar kwa jamii ili kufanikisha jambo hili.

Mwenyekiti wa Zenjydar, bwana Saleh Jaber alisema katika mashindano hayo kuwa, kuwashirikisha na kuwapa watoto fursa ya kuja kuwashirikisha katika mashindano haya yanasaidia watoto na walimu pamoja na wazee kujua maeneo gani watoto wanahitaji kuendelezwa zaidi katika kuisoma Qur'an kwasababu ya makosa madogo madogo yanayotolewa na majaji wanaoaminika wa mashindano hayo. Na zaidi mtoto atakavyoshiriki katika mashindano ndio zaidi anakuwa imara katika kuisoma vizuri Qur'an.

Mmoja wa baadhi ya wazee ambao wamechukua hatua ya kuwasajili watoto wao alipendekeza kuona chuo cha mtoto wake kikifanya mashindano ya watoto wao wenyewe kujua uwezo wa wanafunzi wao angalau mara moja kwa mwaka mpaka watakapofikia katika mashindano ya watoto wote ya Ramadhan Qur'an Contest. Alisema, kufanya hivyo itasaidia kumtayarisha mtoto na waalimu watapata kujua nani wakumtanguliza katika mashindano hayo na wapi makosa yake ili wawasaidie kuwaweka sawa katika makosa hayo madogo.

Mashindano ya mwaka huu kulikuwa na majaji watatu:

Ust. Ali (aliangalia lafdhi na sauti za watoto ambao mshindi wao alituzwa shahada ya kuwa na lafdhi nzuri na mwingine sauti nzuri).

Ust. Sultan (aliangalia 'confidence' na 'appearance' za watoto ambao mshindi wao alituzwa shahada ya kuwa na 'confidence' na mwingine 'appearance').

Ust. Sabry (aliangali Hukmu ambazo ndio kitovu cha Qur'an).

Mshindi wa kusoma Qur'an 2008 aliangaliwa kwa Hukmu zake tu na si kitu kingine. Hukmu zilizowekwa kuangaliwa ni kama zifuatazo:

(الاظهار ,الادغام ,الاقلاب ,الاخفاء ,ميم ساكنة , قلقلة , Ra رَ , Ri رِ , na Shaddah)

Makosa madogo madogo ya washindani ambayo yameonakana na jaji muaminifu, ambayo yamo katika karatasi za jaji, zitafanywa kopi na kila aliyeshiriki mashindano hayo atapata kopi yake aidha kwa kupitia Mwalimu wake ikiwa amewakilisha chuo chake au kwa kupitia kwa mzazi ikiwa amejiwakilisha. Makosa hayo madogo madogo yatasaidia kuwatayarisha watoto vizuri zaidi katika mashindano yajayo. Mwenyekiti wa Zenjydar, bwana Saleh Jaber alisema, vyuo na watoto wote walioshindana wote ni washindi katika mashindano hayo kwa kujiamini kuja kwenye mashindano.

Mwakani tutaanza kutangaza mashindano ya Ramadhan Quran Contest 2009 mapema kama tulivyotangaza mwaka huu kwenye vyuo. Na kwa mzazi yeyote ambaye atapendelea kushiriki katika mashindano hayo anakaribishwa kuleta jina la mtoto wake kwa kujaza fomu ambazo zitatolewa, Ishallah.

Washindi wa mwaka huu ni kama ifuatavyo:

- Mshindi wa kwanza - Rahma Mohammed

- Mshindi wa pili - Omar Salim

- Mshindi wa tatu - Ahmed Salim

- Shahada ya Sauti nzuri - Munawwar Mussa

- Shahada ya Lafdhi nzuri - Omar Salim

- Shahada ya 'Confidence' - Rahma Mohammed

- Shahada ya 'Appearance' - Rahma Mohammed

 

(Kwa maelezo zaidi kuhusu mashindano ya Ramadhan Qur'an Contest wasiliana na bwana Farid Nassor 07951483375 au Saleh Jaber 07886535282)

 

 

Custom Search

Go up

 

Quick Links

Watch Television
Events Calendar
News Archive 2008
News Archive 2007

External Links

Alnoor CET
TZ Embassy UK
TZ's Community UK

© www.zenjydar.co.uk - Since 2007 | Web master | Site map | www.zenjydar.co.uk - Since 2007 ©