Mama Salma azindua
ukarabati sekondari Tabora
29/06/2010

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amezindua
rasmi awamu ya kwanza ya ukarabati na upanuzi (Rehabilitation and
Extension) wa shule ya sekondari ya wasichana ya Tabora unaofanywa kwa
hisani ya Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) kwa gharama
ya zaidi ya shilingi bilioni 1.7. Waliohudhuria uzinduzi huo ni
wanafunzi wa shule za Tabora Wasichana, Tabora Wavulana na Mirambo
pamoja na walimu na Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Abeid Mwinyimsa. |