|
Zenjydar Community Association H Harold Centre, 170 Harold Road, Plaistow, London, E13 0SE È 07886 535282
|
|
TAREHE 21/07/2007 MAFURIKO - UNITED KINGDOM
Wakala wa mazingira wa U.K. wametoa onyo kali la mafuriko katika bara la Midlands (bara lililopo katikati ya U.K.) ambalo mito yake mikuu (Avon, Severn, Dene, Isbourne, Stour na Teme) yalifurika maji kupita kiasi. Pia wameonya wakala hao ya kuwa, baadhi ya maeneo ya Oxfordshire, Berkshire na London, kuna uwezekano wa kunyesha mvua hizo katika siku zijazo. Onyo hilo lilitolewa baada ya sehemu mbalimbali za U.K. kunyeshewa mvua ya miezi miwili kwa muda wa siku moja na kusababisha mafuriko ya maji ambayo yameathiri usafiri na makazi ya wananchi. Waziri Mkuu wa U.K., Bwana Gordon Brown ametamka, mafunzo yamesomwa katika mafuriko yaliyotokea na amesema hatua zaidi zinachukuliwa za kukadiria vipi usafiri na mifereji ya kupitishia maji yaweze kupokea dharura kama hii ambayo si ya kutegemewa iwapo itatokea tena hapo baadaye. Amewasisitiza wakala wa mazingira na wakala wa usafiri kushirikiana zaidi katika kazi zao ili kupunguza athari za maisha ya watu na kazi zao za kila siku. Vile vile amezipongeza huduma za dharura na wanajeshi waokovu kwa kazi nzuri walioifanya katika uokovu wa watu kwenye mafuriko. __________ MATENGENEZO YA UWANJA WA KARUME
__________
__________
Ukarabati wa Uwanja wa Karume ukiwa njiani. Uwanja huo utafanyiwa kuwa ni kituo cha taifa cha soka cha timu za kimataifa na timu za vijana na watoto wa nyumbani kufanya mazoezi yao na kuweka kambi. __________ NGOMA YA PUNGWA
Sherehe za ufunguzi wa Tamasha la Mzanzibari zilizofanyika huko Uroa, mkoa wa kusini Unguja, ambako sherehe za mwaka kogwa hufanyika kila mwaka. Hapo juu ni kikundi cha utamaduni wakicheza ngoma ya Pungwa. __________ TAREHE 22/07/2007 KUPIMA KWA HIYARI
Mheshimiwa Waziri Mkuu wa Tanzania, Bwana Lowasa akijitolea kupima ugonjwa wa ukimwi yeye na mkewe katika kampeni ya kupima kwa hiyari. __________ TAREHE 23/07/2007 MWAKA KOGWA - ZANZIBAR
Mfagia njia __________
Vita vya bakora za majani ya mgomba __________
Leo kazi ipo! __________ TAREHE 24/07/2007 BILL CLINTON NA JAKAYA KIKWETE - TANZANIA
__________ TAREHE 25/07/2007 NAULI YA DALADALA IMEPANDA JUU
Nauli ya daladala na nauli za mabasi ya kwenda mikoani zimepanda kuanzia tarehe 25/07/2007. __________ TAREHE 26/07/2007 TIMU YA VIJANA WA UMRI WA CHINI YA MIAKA 17 YA ZANZIBAR
__________
__________
Timu ya vijana wa umri wa chini ya miaka 17 ya Zanzibar, wakiwa wakijichana na misosi huko mjini Cairo katika ziara ya wiki mbili ya kupiga kambi na kocha wa timu wa kutoka Egypt. Vijana walirudi majuzi ambapo walikuwa katika kambi hiyo wakijitayarisha na kombe la vijana la Afrika mashariki na kati ambalo limedhaminiwa na Rais wa Rwanda, Bwana Pierre Nkurunzinza na kombe limetayarishwa na kutolewa na Rais wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Kikwete. Kila la kheri vijana wetu. __________ LIVERPOOL F.C. WAZINDUA PLAN YA UWANJA MPYA
__________
Liverpool F.C. wamezindua plan ya uwanja wao mpya ambao wanategemea kuanza ujenzi huo hivi karibuni. Uwanja huo ambao una viti elfu sitini, utagharamia £300 milioni (paundi milioni mia tatu za U.K.) na unategemewa kuisha ujenzi wake mwaka 2010. __________
Washabik wa Liverpool F.C., Dar-es-Salaam __________
Tumepitwa na sabasaba mwaka huu. __________ TAREHE 27/07/2007 ZIARA YA BILL CLINTON - TANZANIA
__________
__________
Rais wa 42 wa Marekani, Bwana Bill Clinton alikuwa katika ziara ya siku chache nchini Tanzania katika kampeni yake ya kupigana vita na maradhi ya Malaria na Ukimwi ambayo yanauwa wengi nchini Tanzania na nchi nyingine za Afrika. Ex Rais Clinton amefungua kampeni hiyo ambayo ameipa jina la CHAI (Clinton Foundation for HIV/AIDS). - Picha na Issa Michuzi - Asante Kaka! |
|
|