|
Zenjydar Community Association H Harold Centre, 170 Harold Road, Plaistow, London, E13 0SE È 07886 535282
|
|
|
Usalama wa jiji ulitayarishwa mapema kupambana na yoyote yatakayotokea ambayo yatakayohatarisha usalama wa raia katika kipindi cha Eid-el-hajj, Krismas na mwaka mpya 2007.
Maalim Seif alikutana na wanachama wa CUF katika hotuba yake aliyeitoa akiwepo mjini Northhampton UK, na kujibu maswali yaliyoulizwa juu ya msimamo wa CUF na CCM.
Eid-el-hajj festival 2007, iliandaliwa na Zenjydar Community Association, ikiwa kama ni moja ya siku kuu ya kusheherekea kisa cha nabii Ibrahim (a.s) na mtoto wake Ismail (a.s). Katika tamasha hilo kuliandaliwa na michezo tofauti ikiwamo michezo ya kuigiza ya kiislamu kama ionekanavyo hapo juu pichani. Kisa cha hapo juu ni ustadh Omar Salim akiwaambia wanafunzi wake umuhimu kuhusu sala na kuwafundisha maadili mazuri ya kuwafanya wao waepukane na matendo mabaya kama magenge, madawa ya kulevya, n.k. Ikiwa kama ni mara yetu ya kwanza kuandaa tamasha la Eid, tumefurahi baada ya tamasha kuisha kupokea email na mawazo tofauti kwa njia ya simu kutoka kwa watu tofauti. Na tumeyapokea mawazo yao na vilevile tutayatumia katika tamasha lijalo mwakani. Inshallah.
Ilikuwa ni siku ya furaha kwa watoto na familia nzima
East African Education Foundation na Alnoor Cultural & Education, pia walishiriki katika kuunga mkono fikra ya tamasha hiyo na vilevile jumuiya iliyofika hapo iliwaunga mkono katika kuongeza mfuko wa vyama hivyo. Ilikuwa ni siku ya furaha kwa kila mtu. Kulia ni Ustadh Hafidh wa EAEF, Ustadh Masoud wa Alnoor, Ustadh Sabry wa Alnoor, Ustadh Said wa Alnoor.
Familia zilizofika wakiwa na watoto wao katika tamasha la Eid-el-hajj
Watoto wakiwa katika 'bouncy castle'
Zawadi zilitolewa kwenye steji baada ya maswali na majibu kwa watoto
Majumba ya vioo yazidi kuzagaa mjini Dar
Safari ya maili mia...
Sanamu la bismini lililopo Dar es salaam, limekutwa limefunikwa na mfuko wa plastik kwenye uso wake na kiroba chake cha mgongoni. Ni nani aliyefanya kazi hiyo? Na kamaanisha nini?
Shati kubwa kuliko yote Tanzania, lililopo katika duka moja mjini Dar es salaam, limewekwa kwa kutolewa bure ikiwa kuna mtu litakayemtosha.
Msimu wa matunda hasa mananasi umeanza. Mia tano umekula asali
Waziri mkuu wa zamani wa Pakistan, Benazir Bhutto amefariki dunia katika mji wa Rawalpindi, Pakistan, baada ya mtu aliyesimama karibu na gari lake kujiripua na bomu na kusababisha watu 20 kuuwawa na kujeruhi baadhi ya watu. Miji mingi ya Pakistan ilivurugika kwa ghasia za wananchi kutokana na kifo cha Benazir Bhutto. Habari zaidi bonyeza hapa.
Unguja ilivyo sasa kwa juu
Cheka na vikatuni
- Tutumie picha na habari tofauti za kutoka popote na tutaziweka kwenye mtandao - Email: zenjydar@gmail.com - - Picha za Bongo na Issa Michuzi - Shukran! |
|
|
|