Zenjydar Community Association

H Harold Centre, 170 Harold Road, Plaistow, London, E13 0SE

È 07886 535282

? zenjydar@gmail.com

 

WIKI ILIYOPITA KWA UFUPI

27/10/2007

DARAJA LA RUVU

Ujenzi wa daraja jipya la Ruvu umeanza

Ndani ya viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam, kampeni ya kupiga vita ukimwi inaendelea. Yeyote mpita njia anaweza kwenda humo ndani na akapima na kupata majibu hapo hapo. Kampeni hiyo ilizinduliwa na rais wa Tanzania, mheshimiwa J. Kikwete na kuiita "Tanzania bila ya ukimwi inawezekana".


28/10/2007

ZE COMEDY

Ugomvi wa Joti na Guruguja katika mchezo wa Ze Comedy, Tanzania

KINGWENDU

Huyu ndie Kingwendu ambaye wengi wenu mnamjua katika michezo yake ya kuchekesha, ni mchekeshaji mwenye kipaji ambacho akitokea kabla hajakuchekesha, utacheka.


29/10/2007

MATANGAZO LAIVU

Matokeo: Liverpoo 1-1 Arsenal


30/10/2007

JENGO LA MAGEREZA

Jengo ambalo litakalokuwa makao makuu mapya ya jeshi la magereza ambalo lipo mtaa wa Shaaban Robert/Sokoine Drive mjini Dar es Salaam

AIRBUS A380

Kaka Issa Michuzi katuletea picha mpya za ndege kubwa ya kwanza yenye kuchukua abiria juu na chini na yenye raha zote za kila aina ambazo utazihitaji. Urefu wa A380 kwenda juu ukichukulia na upanga wake ni sawasawa na ghorofa sita. Hii ni picha yake kwa nje.

Matairi

Ndani

Ndani

Ndani

Ndani

Ndani

Kaka Issa Michuzi akionekana yupo ndani ya pipa


30/10/2007

MISS TANZANIA 2007

Waziri wa mambo ya nje na uhusiano wa kimataifa, Mh. Bernard Kamilius Membe, anamkabidhi Miss Tanzania 2007 Richa Adhia, bendera ya taifa katika hafla ya kumuaga kwenda kushindana mashindano ya Miss World 2007. Mashindano ya Miss World 2007 yatafanyika China katika mji wa Sanya, tarehe 1/12/2007.

DAMU NZITO

Familia iliyopo hapa Uingereza wamebahatika kupata watoto wawili mapacha kurwa na dotto ambao kwa uwezo wake mola, mtoto mmoja katoka mzungu na mmoja katoka mmatumbi pyua. Wataalam wanasema hii hutokea kwa nadra sana; mara moja katika milioni moja.


31/10/2007

SHOPPERS PLAZA

Shoppers Plaza ni moja ya supermarket kubwa zilizopo Dar es Salaam. Ipo barabara ya Old Bagamoyo road ukielekea Mikocheni.

KLABU YA BILICANAS

Klabu maarufu ya Bilicanas ikionekana ikiwa katika ukarabati wa muda mrefu wa kuitanua na kuitengeneza klabu hiyo iwe ya kileo zaidi mjini Dar es Salaam.


01/11/2007

YANGA YAFUNGIA WACHEZAJI

Klabu ya Yanga ya Dar es Salaam, Tanzania, imewafungia wachezaji wake kwa muda wa miezi sita na baadhi yao kufungiwa kwa miezi mitatu kwasababu ya utovu wa nidhamu. Wachezaji hao ambao walitoroka kambini baada ya mechi yao na Simba. Waliofungiwa kwa miezi sita ni Ivo Mapunda na Shadrack; na waliofungiwa miezi mitatu ni Ben Mwalala na Edwin Mukenya.

Shadrack Nsajigwa

Edwin Mukenya

Ben Mwalala

HUDUMA ZA TRENI ZAANZA TENA

Baada ya takriban mwaka mmoja, treni ya abiria ya kwenda mikoani ilisimama kwasabuabu fulani fulani. Leo imeanza huduma zake tena rasmi kuelekea Mwanza na Kigoma kutoka Dar es Salaam na jamaa na ndugu wa abiria wakionekana pichani wakiaga jamaa zao wanaoelekea mikoani.

Baadhi ya wakubwa wa shirika la treni walikusanyika kuiaga treni hiyo ikiwa ikiondoka kwa kuanza huduma zake kuelekea mikoani.

Abiria wakionekana wakiaga ndugu na jamaa zao


02/11/2007

MALIASILI NA UTALII

Jengo jipya ambalo litakuwa makao makuu mapya ya wizara ya Maliasili na Utalii liliopo barabara ya Nyerere (zamani pugu road) linakaribia kuisha.

KATUNI

Cheka na vikatuni


- Tutumie picha na habari tofauti za kutoka popote na tutaziweka kwenye mtandao - Email: zenjydar@gmail.com -

- Picha za Bongo na Issa Michuzi - Shukran!

© www.zenjydar.co.uk