|
Zenjydar Community Association H Harold Centre, 170 Harold Road, Plaistow, London, E13 0SE È 07886 535282
|
|
TAREHE 01/09/2007 HESHIMA KWA NYOTAZ WA ENZI ZAO
Enzi zao! Peter Tino akionekana pichani akitia saini mpira maalum ambao wachezaji wote wa zamani wa taifa stars walitia saini katika mpira huo ambao ulitolewa maalum na kampuni ya vifaa vya michezo vya AB sports. Kampeni ya mkutano huo uliofanyika Sea Cliff, ni moja ya kuwapa moyo wachezaji wapya wa taifa stars ili wafanye vizuri katika mashindano yao. Peter Tino alikuwa ni mshambuliaji hatari wa timu ya Pan Africa na vilevile alichezea taifa stars. Tino yupo kwenye vitabu vya historia baada ya kuifikisha bongo kwenye fainali za Afrika huko Lagos, Nigeria, mwaka 1981 kwa goli lake pekee alilowafunga Zambia. Kwa mbali nyuma, mwenye nyekundu, ni Ahmed Amasha ambaye alikuwa beki tatu hatari wa timu ya Yanga na taifa stars (aaaahh!! enzi hizo!) na baadaye alihamia Muscat, Oman kuchezea timu ya Fanja.
Peter Tino na Kitwana Manara
Peter Tino akisalimiana na makocha wa taifa stars. Kulia ni kocha wa vijana Tinocco, akifuatiwa na kocha wa viungo Ittamar na Kitwana Manara akishuhudia.
Kulia chini ni Sekilojo Chambua, Mwenyekiti wa Yanga, Imani Madenga na Makumbi Juma "homa ya jiji". Waliosimama ni Romario, Mohamed Hussein, Kombo na Abubakar Salum "sure boy".
Kushoto ni Juma Pondamali Mensah ambaye alikuwa Tanzania One wa enzi hizo. Kushoto ni Tanzania One wa sasa Ivo Mapunda
Mohamed Hussein "Mmachinga" akiwa na vijana wa taifa stars
Makocha wa taifa stars wakiwa na wachezaji wa zamani wa taifa stars. Kushoto waliosimama ni Othman Juma Chama, Sunday Manara, Mwankemwa (Daktari wa timu), Richard Adolf, Mtemi Ramadhan, Maximo, Mohamed Mkweche, Isihaka Hassan "Chuku", Ahmed Amasha, Ittamar, James Kisaka, Tinocco, Kitwana Manara na aliyekaa chini ni Juma Pondamali.
Kushoto ni mbunge wa Kinondoni mheshimiwa Iddi Azzan akiwa na bosi wa kampuni ya Easy Finance mheshimiwa Isaac Kasanga na mgunge wa Mafia na Abubakar Salum "sure boy". __________ MASHINDANO YA SHARUBU
__________
__________
_________
Mashindano ya dunia ya kutafuta mshindi wa usanii wa masharubu na ndevu ya mwaka 2007 yalifanyika mjini Brighton, Sussex, England. Washindanaji walitoka nchi tofauti zikiwamo Hungary, Romania, Zurich, Marekani, Greece, Italy, n.k. _________ MENO YA CHUMA
__________
__________
Rathakrishnan Velu, ni mtu wa Malaysia ambaye anajulikana kwa jina lingine kama "King Tooth" alivunja rekodi ya dunia baada ya kuvuta treni ambayo ina mabehewa saba kwa kutumia meno yake ya kuzaliwa nayo na kamba ya waya za chuma. __________ TAIFA STARS YAPAMBANA NA UGANDA CRANES
Tiketi ya kuingilia uwanja mpya wa taifa katika mechi ya kirafiki baina ya taifa stars na Uganda cranes
Mlangoni, skauti wakisaidia kuwaruhusu watu kuingia kwenye mechi
Fanya fujo uone! Jeshi la kujenga taifa walipewa kazi ya kuangalia usalama katika wanja jipya la taifa
Kwa utaratibu kabisa
Na kwa mpango kabisa
Washabiki
Washabiki
Washabiki
Washabiki
Washabiki
Washabiki
Washabiki
Parking
Walete walete!
Taifa Stars
Uganda Cranes
Waamuzi: kushoto ni kamisaa wa mechi Maulid Dilunga na katikati ni mwanamke wa kwanza wa kibongo kupata beji ya FIFA.
Mheshimiwa JK akimwaga vitu laivu kwenye waidi skrini. Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete ndiye Rais wa kwanza kutilia mkazo na kujihusisha sana kwenye mambo ya kuendeleza michezo nchini Tanzania.
Vyombo vya habari
Wasikwambie hujafika
Abesi-abesi. Katika mechi hiyo, Taifa stars walishinda bao 1-0 katika dakika ya 20 ya kipindi cha pili. __________ MISS TANZANIA 2007
Richa Adhia, ndiye Miss Tanzania 2007 baada ya kuchuana na washindani wengine huko Dar es Salaam katika hoteli ya Beach Comber katika usiku wa tarehe 01/09/2007.
Katuni ya kwenye gazeti la bongo
Kumi bora
Tano bora
katikati balozi wa Palestina akimpa zawadi Richa Adhia ambaye ni Miss Tanzania 2007. Kulia kabisa ni Miss World 2001 Agbani Derago, ambaye alikuwa ni jaji mkuu katika mashindano hayo. 02/09/2007 WABONGO WA HOUSTON NA ATLANTA - MAREKANI
Timu ya wa Tanzania waliopo Atlanta, Marekani
Timu ya wa Tanzania waliopo Houston, Marekani. Timu ya Houston waliifunga timu ya Atlanta mabao 5-3 katika mechi za kirafiki 03/09/2007 KIMOMBO
Boda kwa boda; Bongo, hakuna kisichowezekana __________
Boda kwa boda, vitu Laivu tuuuu!!! _________
__________
__________
Basi maarufu la U.K. "National Express" linaonekana likilala kiubavu baada ya kuachia njia kuu ya "motorway" (M1). Basi hilo ambalo lilikuwa limebeba abiria karibu 30, lilikuwa linatoka Birmingham na kuelekea Luton mpaka Stansted Airport, baada ya ajali hiyo kutokea dereva aliwekwa chini ya ulinzi baada ya kushukiwa kuwa alikuwa amelewa na huku akiwa akiendesha basi la abiria. Baadhi ya abiria ambao wamepona, mmoja wao alisema aliliona basi likiwa likiyumbayumba mara mbili tatu na aliamua kufunga mkanda wake ambao anadai ndio ulimsaidia kuepuka na kupata majeraha. 04/09/2007 MAENDELEO YA AFYA ZANZIBAR
Waziri wa afya na huduma za jamii wa Marekani akiongozwa na maofisa wa Zanzibar katika kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo visiwani Zanzibar. __________
Basi la taifa stars limeshanolewa na linangoja kuchukuwa wachezaji kupambana na Msubiji siku ya Jumamosi tarehe 08/09/2007 huko Dar es Salaam. 05/09/2007 BODA KWA BODA
Boda kwa boda __________
Boda kwa boda __________
Boda kwa boda, Morogoro __________
Boda kwa boda, Mbeya. __________ SPIDER MAN - NDANI YA URUSI
__________
__________
__________
__________
Alain Robert, ambaye anajulikana kwa jina la "Spiderman" alionyesha umahiri wake kupanda jumba jipya la (Federal Tower) lililopo Moscow, Urusi, ambalo lina urefu wa futi 720. Alain (45) hutumia mapendekezo yake hayo bila ya kutumia vifaa vyovyote vya usalama vya kumzuia ili asianguke ikiwa atateleza akiwa juu, vilevile hufanya hivyo bila ya kuomba ruhusa ya vyombo vya sheria na hufanya kujifurahisha yeye mwenyewe tu! Alain ambaye ni Mfaransa, alianza "hobby" yake hiyo tangu akiwa na miaka 12 wakati aliposahau funguo za nyumbani kwao ndani ya nyumba yao na alipanda jumba walilokuwa wakikaa ghoroga ya nane kuzifuatia funguo hizo, na tangu siku hiyo ndio ikawa kama mchezo. Alain ameshawahi kupanda Eiffel Tower iliyopo France na Opera House iliyopo Sydney, Australia. 06/09/2007 TEMBO WA USANII WA MAJITI NDANI YA LONDON
__________
__________
__________
__________ Tembo ambao walitengenezwa kwa majiti walionekana wakiwa katika bustani maarufu ya Hyde Park, London 07/09/2007 SHIRIKISHO LA VYAMA VYA UPINZANI
__________
__________
__________
Viongozi wa kutoka vyama tofauti nchini Tanzania walifanya mkutano wa hadhara mjini Mbeya. Mkutano huo ulikuwa ni mkutano wa shirikisho la vyama vya upinzani vikiwemo TLP, CHADEMA, CUF na NCCR. __________ TAARIFA YA RAIS WA TANZANIA MHESHIMIWA KIKWETE YA TAREHE 14/08/2007 JUU YA CCM NA CUF
Taarifa ya Rais wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, ambayo aliitoa siku ya tarehe 14/08/2007, Ikulu, Dar es Salaam juu ya maelewano ya vyama viwili hivyo (CCM na CUF). JK alisisitiza kuwa yeye ni mwenye shauku kubwa ya kuleta mapatano na maendeleo ya kuafikiana baina ya vyama hivi na alikisisitiza chama cha (CUF) na uongozi wa chama hicho akiwemo Profesa Ibrahim Lipumba kuwa kujitoa katika maongezi hayo hakutoleta maendeleo ya maelewano. JK alieleza kuwa ataendelea kuleta maendeleo ya maelewano kati ya vyama hivyo na alikumbusha chimbuko la mazungumzo hayo ni ya ahadi aliyoitoa kwa Watanzania katika bunge tarehe 30 Disemba 2005. Alisema katika taarifa yake, anaamini kwa dhati ya moyo wake kuwa hakuna tofauti zozote za kisiasa na kijamii katika nchi yetu zisizomalizwa kwa mazungumzo na anaamini mpasuko huo wa kisiasa unaweza ukawafikiana ikiwa vyama hivyo vitakaa pamoja na kuzungumzia tofauti zao. JK alisema katika taarifa hiyo, mpaka sasa wameshakaa vikao vingi vya maelewano na wameshaelewana katika sehemu tofauti za mazungumzo yao na anaamini kuna sehemu chache tu zilizobakia ambazo pia zinaweza kumalizwa kimazungumzo. Rais Kikwete alisema, mpasuko huo wa kisiasa unaweza ukatatuliwa kimazungumzo ya maelewano ya pande zote mbili; na kama mpasuko huo ukiendelea bila ya mazungumzo, tutarudi kule tulikokuwa, yaani kwenye uhasama, shutuma zisizoisha, kubaguana, kutozikana na hata kutosalimiana. Itakuwa tutaendelea na utamaduni mbaya wa kuzifanya tofauti zetu za kisiasa kuwa ni chanzo cha uadui, chuki na hivyo kuhatarisha amani, utulivu na umoja wa taifa letu na watu wake. Taarifa kutoka Ikulu, Dar es Salaam, tarehe 14/08/2007 __________ JK NA TAIFA STARS
Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete akitia sahihi kwenye mpira akiwa na rais wa TFF Leodgar Chilla Tenga alipotembelea kambi ya taifa stars katika hoteli ya Golden Tulip. __________
Mheshimiwa Kikwete akipokea mpira ambao umesainiwa na wachezaji wote wa taifa stars. Anyempa mpira huo ni Mwenyekiti wa bodi ya kampuni ya Serengeti, Mheshimiwa Jaji Bomani. __________
Kikwete akichangamsha baraza kidogo kwa kuwapa moyo vijana wa taifa stars katika mechi yao ya kesho tarehe 08/09/2007, na timu ya taifa ya Msumbiji ambayo itafanyika Dar es salaam. JK aliwaambia vijana kuwa ana matumaini kuwa kesho vijana watashinda na ushindi utakuwa mtamu, lakini ya mungu mengi. Katika mazungumzo yake alisema kuwa yeye atakwenda Arusha kikazi lakini kama akimaliza mapema atarudi kuja kushangilia na rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Amani Abeid Karume atakuwepo kuongoza mashabiki katika ushangiliaji. __________
JK akipozi na timu ya taifa stars katika kuwapa moyo na mechi ya kesho na Msumbiji. JK akionyesha kujihusisha kwake katika maendeleo ya michezo nchini ambayo yeye mwenyewe ameyasisitiza. JK alipitia kambini hapo moja kwa moja alipotoka Kondoa katika ziara yake ya kikazi. __________
Bango la kushabikia taifa stars likionekana waziwazi katika mitaa ya jijini Dar es salaam na pichani ni kaka Issa Michuzi akionyesha uzalendo wake katika pozi ya stamina kwa kusimama na mguu mmoja. Kaka uko fitiiiiii! - Picha za Bongo na Issa Michuzi - Shukran! |
|
|