|
Zenjydar Community Association H Harold Centre, 170 Harold Road, Plaistow, London, E13 0SE È 07886 535282
|
|
TAREHE 08/09/2007 TAIFA STARS NA MSUMBIJI
Baada ya kungoja kwa hamu na kwa siku nyingi mechi ya mpira wa miguu baina ya taifa stars a na timu ya taifa ya Msumbiji, ile siku imefika (tarehe 08/09/2007). Mgeni wa heshima alikuwa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Amani Abedi Karume. Matokeo ni Tanzania 0 Msumbiji 1. Bado kuna kazi kubwa ya kufanywa. __________
Matumaini yanaanza kuondoka baada ya kufungwa bao 1-0 __________
Washangiliaji wote wamekwisha nguvu baada ya kuona dakika za mwisho zinawadia na hakuna matarajio yoyote __________ AJALI YA BASI - MBEYA
Basi la abiria la SABCO lililokuwa liktoka Tunduma kuelekea Dar es Salaam lilipata ajali na lori la kubebea mchanga lilipovaana uso kwa uso na kupoteza maisha ya watu zaidi ya watu 28 na kujeruhi zaidi ya watu 30. Ajali hiyo ilitokea katika kijiji cha Igurusi, wilaya ya Mbarali, Mbeya. Katika ajali hiyo alikuwamo muimbaji maarufu Shenazi Salim (33) pichani chini, ambaye alikuwa akitokea Mbeya na basi la SABCO.
Shenazi kazikwa tarehe 11/09/2007 __________
Hili ndilo gari lililobeba mchanga lililogongana na basi la SABCO huko Mbeya __________
Majeruhi __________
Mmoja wa waliojeruhiwa akihojiwa na polisi ili wapate utambulisho wake TAREHE 09/09/2007 MASHINDANO YA KUMENYA VIAZI
Mashindano ya kumenya viazi yaliyofanyika Mbeya katika uwanja wa Sokoine TAREHE 10/09/2007 UZALENDO
Uzalendo TAREHE 11/09/2007 BALOZI NCHINI UAE
Balozi wa Tanzania nchini U.A.E, Mheshimiwa Mohamed Maharage (mwenye tai nyekundu) alikuwamo katika mmoja wa mabalozi kumi walioalikwa rasmi katika mualiko aliouandaa Mfalme wa Abu dhabi, Sheikh Khalifa Bin Zayed Al Nahyan __________ AJALI MJINI - DAR ES SALAAM
Ajali ya magari yaliyokwaruzana katika mtaa wa Samora na kusababisha msongamano wa magari, Dar es salaam TAREHE 12/09/2007 KUKARIBISHA MWEZI MTUKUFU
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la mapinduzi, Mheshimiwa Amani Abeid Karume akitoa hutuba ya kuukaribisha mwezi mtukufu wa Ramadhan huko ikulu ya Zanzibar TAREHE 13/09/2007 MWEZI MTUKUFU WA RAMADHAN
TAREHE 14/09/2007 MLIMA WA KITONGA
Huu ndio mlima maarufu wa Kitonga nchini Tanzania. Kitonga unasemekana una kona 32 kama uzionavyo pichani mpaka kufika chini au kileleni. Kama dereva kazi kwako. - Picha za Bongo na Issa Michuzi - Shukran! |
|
|