|
Zenjydar Community Association H Harold Centre, 170 Harold Road, Plaistow, London, E13 0SE È 07886 535282
|
|
TAREHE 15/09/2007 MHESHIMIWA MUDHIHIR MUDHIHIR
Mbunge wa Mchinga mheshimiwa Mudhihir Mudhihir alitembelewa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili mjini Dar es Salaam na waziri wa usalama wa raia mheshimiwa Harith Bakari Mwapachu. Mheshimiwa Mudhihir alilazwa hospitali ya Muhimbili baada ya kupata ajali ya gari huko mkoani Lindi ambayo ilisababisha akatwe mkono wake wa kulia. __________
Mheshimiwa Jakaya Kikwete akimuapisha luteni jenerali Abdulrahman Shimbo kuwa Mnadhimu mkuu wa jeshi __________
Mheshimiwa Jakaya Kikwete akimuapisha mkuu mpya wa majeshi jenerali Davies Mwamunyange TAREHE 16/09/2007 SANAMU KARIBU NA LONDON BRIDGE
__________
__________
Sanamu la muogeleaji ambalo limeshindiliwa ardhini katika ufukwe wa kusini mwa mto Thames, London, karibu na daraja maarufu la 'London Bridge' ambalo tangu liwekwe limevutia wapita njia wengi wakiwamo wakazi na watalii wa London. Sanamu hilo limetayarishwa kutangaza kipindi maalum ambacho kitakuwa kinaonyeshwa katika kipindi cha Discovery Channel kila Jumapili, saa nne usiku kuanzia tarehe 23/09/2007. __________
Sanamu lingine limewekwa katika 'concourse' ya Victoria station TAREHE 17/09/2007 HESHIMA NI KITU CHA BURE
Mheshimiwa Augustine Mrema (pichani juu) akionekana akimpa mkono wa heshima rais wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Kikwete. Mbali na kuwa ni wapinzani wa vyama, lakini inadhihirisha kuwa tuna utamaduni mzuri wa kiungwana na wa kibinadamu ambao tumekuwa nao katika nchi yetu ya Tanzania. TAREHE 18/09/2007 DAR ES SALAAM
Hili ni moja ya majengo yanayopendezesha Dar es Salaam hivi sasa __________ AFANDE
kuwa afande inalipa samtaimu! 19/09/2007 NYANGUMI MJINI PAJE - ZANZIBAR
Wakazi wa kitongoji cha Paje, Zanzibar, wakijipatia rizki ya mafuta ya nyangumi ambaye alikutwa pembeni mwa bahari. Inasemekana, mafuta ya nyangumi ni dawa ya maradhi tofauti ambayo hutumika huko nyumbani. __________ KAZI NI KAZI
Kumbuka! Kazi ni kazi tu popote pale ulipo! 20/09/2007 MATT DAMON NA BEN AFFLECK NDANI YA TANZANIA
Wasanii maarufu katika filamu za Hollywood, Matt Damon (kulia) na Ben Affleck (wa tatu kutoka kulia mwenye t-shirt nyeupe) walikuwa Tanzania katika matembezi yao ya kusaidia mayatima. __________ 21/09/2007 KITUO CHA MNAZI MMOJA
Kituo cha basi cha Mnazi Mmoja cha kubebea abiria haraka-haraka kionekanavyo hivi sasa. __________ KATUNI
Cheka na vikatuni __________
Hii sio katuni - Picha za Bongo na Issa Michuzi - Shukran! |
|
|