|
Zenjydar Community Association H Harold Centre, 170 Harold Road, Plaistow, London, E13 0SE È 07886 535282
|
|
TAREHE 22/09/2007 HALI YA HEWA YACHAFUKA DUNIANI
Watu kumi na tano wamekufa kwa kuzama kwenye mafuriko yaliyoikumba Kenya na kuua watu mia mbili katika nchi tofauti za Afrika ambazo zimekumbwa na mafuriko hayo. Pichani juu, ni kijiji cha Budalangi, mashariki mwa Kenya. __________
__________ UGANDA
__________
Uganda imepatwa na mafuriko na kuathiri makazi ya wananchi. Baadhi ya wakazi wakionekana wakivuka mto Aswa uliopo kaskazini mwa Uganda. __________ SLOVENIA
__________
Slovenia pia imepatwa na mafuriko na inasemekana watu wanne wamekufa kwa kuzama na maji na wengine kupotea baada ya mafuriko kuyakumba mji wa Zelezniki ambao upo maili 30 kutoka mji mkuu wa Slovenia, Ljubljana. Slovenia haijawahi kupata mafuriko ya namna hiyo zaidi ya miaka thelathini. __________ ENGLAND
__________
__________
__________
Baadhi ya sehemu za kusini na sehemu kanda ya kati ya England zilikumbwa na kimbunga cha nguvu ambacho kiliathiri makazi ya watu, magari na kuchimbua miti na mapaa ya nyumba. TAREHE 23/09/2007 HOTELI YA SEA CLIFF DAR ES SALAAM YAUNGUA
__________
__________
__________
__________
Hoteli ya Sea Cliff iliyopo Dar es Salaam, ambayo ilitengenezwa kiutamaduni na mapaa ya makuti, imeungua asilimia 75 ya makuti hayo na kuicha hoteli hiyo nyang'a nyang'a. Moto huo ambao unasemekana ulianzia aidha jikoni au chumba cha wafanyakazi, ulianza tangu saa kumi na mbili za jioni mpaka kufika kwa wana zima moto na kuutuliza moto huo kwenye mida ya usiku. Hakuna aliyejeruhiwa wala aliyekufa. TAREHE 24/09/2007 SEA CLIFF HOTEL - HIVI LEO
__________
__________
__________
__________
__________
Hoteli ya Sea Cliff, baada ya kuungua sana! TAREHE 25/09/2007 KIKWETE ASISITIZA MUUNGANO WA WATANZANIA POPOTE PALE WALIPO
Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, mheshimiwa Jakaya Kikwete akizungumza na watanzania nane waliopo Marekani katika hoteli ya Grand Hyatt, New York. JK alizungumzia kuundwa chombo na jitihada za kuunganisha watanzania wote waliokuwapo nje na Tanzania __________ KARIAKOO
Mtaa wa Swahili na Msimbazi, Kariakoo, Dar es Salaam, ionekanavyo hivi leo. TAREHE 26/09/2007 TRAFIKI KAZINI
Trafik akionekana kujaribu kuzishtua-shtua taa za barabarani ambazo zilizokuwa zikileta mushkeli kidogo. __________ DAR ES SALAAM SKYLINE
Sura ya Dar inaanza kubadilika na maendeleo yanashamiri. 27/09/2007 MHESHIMIWA KIKWETE AKIHUTUBIA KATIKA UMOJA WA MATAIFA
Rais wa Tanzania akihutubia umoja wa mataifa huko Marekani. Kwa ripoti kamili ya Mheshimiwa, dokoa hapa. 28/09/2007 TUJIKUMBUSHE ENZI HIZO
Huyo ni mshabiki wa Simba alikuwa akijitokeza na mbuzi zake kwenye mashindano makubwa ya wakati huo baina ya Simba na Yanga za Tanzania. Pichani ni uwanja wetu wa taifa ulivyokuwa zamani. KARATE
Cheka na vikatuni - Picha za Bongo na Issa Michuzi - Shukran! |
|
|