|
Zenjydar Community Association H Harold Centre, 170 Harold Road, Plaistow, London, E13 0SE È 07886 535282
|
|
TAREHE 29/09/2007 JOSEPH NA JOSEPHINE
__________
__________
__________
__________
__________
Joseph na Josephine walikuwa wachumba wa muda mrefu huko Marekani ambao waliwekeana ahadi ya kuwa pamoja maishani. Joseph alipata nafasi ya kupelekwa Iraq kupigana vita. Katika harakati za vita, kikundi cha Joseph kilipigwa bomu na Joseph alijeruhiwa na kuunguwa vibaya sana mwili mzima. Inavyosemekana, jinsi unavyomuona usoni ni afadhali kuliko maungo yake mengine ya ndani ya mavazi yake. Lakini pamoja na hayo yote, Josephine alikuwa tayari kuwa na mpenzi wake aliyeweka naye ahadi ya kuwa naye maishani milele na kukubali kufunga nae pingu za maisha. Ama kweli ahadi ni kitu kikubwa kwa yule anayeiweka moyoni. TAREHE 30/09/2007 JELA YA AUSTRIA
__________
__________
__________
__________
__________
__________
__________
__________
__________
__________
__________
Picha za hapo juu ni za jela ya Austria 01/10/2007 URAIA WA NCHI MBILI
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Bernard
Membe, amesema serikali itahakikisha sheria ya uraia wa nchi mbili
inapitishwa kwa manufaa ya Watanzania na taifa na si vinginevyo. Habari na Mobhare Matinyi, New York. __________ JK NDANI YA NEW YORK
Mheshimiwa Jakaya Kikwete akipokea mpira kutoka kwa mmoja wa watanzania wanaoishi Marekani. 02/10/2007 MLIMA WA KILIMANJARO
Mlima wetu wa Kilimanjaro uonekanavyo hivi sasa. __________ DOKTA ALIPITIWA KIDOGO!
Daktari wa kienyeji alipitikiwa na usingizi kidogo alipokuwa kazini. __________ MTAA WA SAMORA
Huu ni mtaa wa Samora Avenue uonekanavyo hivi sasa. __________ BIG BEN YAVUMA TENA
__________
__________
__________
__________
__________
__________
__________
Saa maarufu duniani yenye kengele ya Big Ben ambayo ipo Westminster, imerudi tena ulingoni baada kufanyiwa matengenezo muhimu. Kengele hiyo iligonga kwa mara ya mwisho tarehe 11/08/2007 kwa matengenezo hayo ya karibu miezi miwili na kuanza kuwika tena katikati ya jiji la London. Mwaka 2009, Big Ben itasheherekea miaka 150 tangu ianze kazi yake. Kwa habari zaidi ya Big Ben, dokoa hapa. __________ 03/10/2007 UWANJA WA NDEGE - DAR ES SALAAM
Uwanja wetu wa ndege wa taifa uliopo Dar es Salaam. __________
Uwanja wetu wa taifa ukiwa katika kumaliziwa na matengenezo madogo madogo. 04/10/2007 NEMBO MPYA YA AIR TANZANIA
Hio ni moja wa mfano wa nembo za ndege zetu mpya zitakavyokuwa. Air Tanzania wameagiza baadhi ya ndege kutoka Airbus (shirika la utengenezaji ndege) ili kutanua huduma zake. __________ STESHENI
Kituo cha daladala cha stesheni kikionekana hivi sasa. Kwa mbali ni jengo la Kastam. 05/10/2007 MAENDELEO YA UWANJA WA KARUME
Uwanja wa Karume ukionekana umemwagiwa changa la kutiwa nyasi feki za kimataifa. Maendeleo hayo ni moja ya kuutengeneza na kuutayarisha uwanja wa Karume kwa mazoezi ya timu ya taifa na vijana. __________ SKILLS
Kijana akionekana katika mitaa ya Dar es Salaam akionyesha utundu wake wa kuziruka baiskeli huku akiwa amevaa roller skates au (viatu vya magurudumu). __________ ENZI ZAO!
Haidar Omar Abeid (Muchacho) ambaye alikuwa kepteni wa timu ya Simba akipokea kombe la ubingwa ambalo Simba walijinyakulia katika ligi kuu ya mwaka 1975. Haidar hivi sasa anaishi uarabuni. __________ KATUNI ZA ZAMANI
Cheka na vikatuni. - Picha za Bongo na Issa Michuzi - Shukran! |
|
|